
*****SORY MADAM*****(14)
“Hapana mama sijasema kitu chochote”
“Ujasema kitu chochote wakati umezungumza hicho ulicho kizungumza?”
“Mama tupotezee hiyo mada”
“Eddy Eddy wewe lete huo ujinga wako tuu na ole wako nichunguze hilo swala alafu nijue ni kweli oune jinsi itakavyokuwa kama sintokufunga”.
Mama alizungumza kwa hasira huku akishuka ndani ya gari na kuelekea sehemu aliyoingizwa Manka.Sikujua atakwenda kuzungumza nani ikanilazimu nishuke ndani ya gari na kumfwata kwa haraka,nikamkuta mama amesimama na Manka huku akimuonya.
“Nisikie siku una uhusiano na mwangangu utanitambua mimi ni nani hapa si anajifanya anakutetea ila ukiingia ndani ya mikono yangu utajuta kuzaliwa”
“Mama mbo……”
“Tena na wewe funga bakuli lako nenda nikukute kwenye gari”
“Lakini mam……”
“Hakuna cha lakini nimekuambia funga bakuli lako na sihitaji uzungumze upumbavu wowote sawa.Angekuua huyo ndio ungefurahi si ndio?”
“Ila mama si nimeshasema Manka hausiki na kitu chochote”.
Mama akanitazama kwa jicho la hasira kisha akanisonya na kutoka huku akitembea kwa hatua ndefu kurudi kwenye gari huku mlinzi wake akimfwata kwa nyuma akimtuliza jazba.Wakati wote mama alipokuwa akizungumza Manka alikuwa ameinama chini huku analia kwa uchungu,nikamsogelea taratibu na kumkumbatia japo mikono yake imefungwa pingu kwa mbele.
“Eddy niache tu nikafungwe mama yako amesha tengeneza chuki juu yangu”
“Manka ni maneno gani unayoyazungumza eti?? sipo tayari iwe kama hivyo nahitaji utulize akili katika hili nakuomba tena sana mmmm”
“Eddy hata nikiwa huru sintoweza kuwa na uhuru kama mwazonni….Laiti baba yangu angekuwapo nisinge nyanyasika kiasi hichi”
“Kwani baba yako nyupo wapi?”
“Ni historia ndefu Eddy ila kwa ufupi baba yangu ana uwezo mkubwa wa kiuchumi ila alimtelekeza mama baada ya kunizaa mimi……….ila sijui ni wapi alipo japo ninasikia sikia amepandishwa cheo kazini kwake”
“Ulisha wahi kukutana naye hizi siku za karibuni?”
“Hapana mara ya mwisho kukutana naye nilikuwa na umri wa miaka mitano kuanzia hapo nina msikia sikia”.
Nikajikuta ninapata maumivu mengi moyoni mwangu huku mawazo ya kwa nini baba anafanya hivi yakitawala kichwani mwangu.
“Eddy mama yako anachokizungumza ni kweli nakuomba uniache nikafie jela”
“Manka acha kuzungumza kitu kama hicho ila tambua kuwa nipo upande wako hadi dakika ya mwisho”.
“Eddy mama yako anachokizungumza ni kweli nakuomba uniache nikafie jela”
“Manka acha kuzungumza kitu kama hicho ila tambua kuwa nipo upande wako hadi dakika ya mwisho”.
Nilizungumza na kuondoka na kumuacha Manka akibaki ananishangaa.Muda wa kuingia mahakamani ukawa tayari umesha wadia sikuhona haja ya kumsubiria mama kuingia naye kwenye ukumbi wa mahakama nikatangulia mwenyewe na kumkuta mwalimu Mayange na familia yake wakiwa wamekaa kwa masikitiko.
“Eddy”
Mwalimu Mayange liniita na nikamfuata katika sehemu waliyokaa.
“Eddy mwanangu nakushukuru kwa masaada wako japo tunasubiria majibu ya mahakama”
“Usijali mwalimu Mungu atasaidia yatakwisha”
“Kumbe mama yako ni waziri?”
“Ndio”
“Hongera”
“Asante”.
Nikaondoka na kwenda kukaa katika eneo nililokuwa nimekaa mwazoni na baada ya muda kesi ikaanza,kutokana muhusika mkuu nilikataa Manka kuwa sio muhusika ikalazimika kesi kufutwa na Manka kuachiwa huru.Upande wa familia ya Manka ikatawaliwa na furaha ila kwa upande wangu mama amekasirika.
“Kwenye gari langu hupandi na utakuja kwa miguu”
“Mama….
“Hakuna cha mama, Zuhura hebu mpe alfu ya daladala”
“Sawa bosi”
Mlizi wa mama akafungua kipochi chake na kunipa alfu moja ya daladala kisha wao wakaingia ndani ya gari na wakaondoka nikabaki nimesimama ninawashangaa kwani sikuamini kama mama anaweza kunifanyia kitu kama hicho.Nikiwa bado sijui cha kufanya nikasikia sauti ya Manka ikiniita kwa nyuma nikageuka na kumkuta amesimama huku akiwa na tabasabu usoni mwake.
“Eddy nashukuru kwa msaada wako yaani sijui hata nikushukuruje”
“Usijali best yangu”
“Ila Eddy nina zawadi yako kama nilivyokuambia pale mwazoni”
‘Una zawadi gani?”
“Nina ujauzito wako”Kusema kweli mapigo ya moyo nikahisi yamepoteza muelekeo na kunifanya mwili mzima kuanza kuzizima kiasi kwamba jasho likaanza kunimwagika huku mdomo ukiwa mzito kuzungumza kitu ninacho taka kukizungumza hadi Manka akahisi kitu.
“Eddy una tatizo?’
“Hapana…..mnarudi Arusha leo?”
“Ndio ninamsubiria shemeji aje kutuchukua amelipeleka gari gereji”
“Ahaa basi Mungu akibariki hilo swala la mtoto tutakuja kulizungumza huko Arusha”
“Lakini mbona unaonekana kama huna furaha nilivyokuambia kuwa mimi ni mjamzito?”
“Haaa nimefurahi ila tutatafuta muda tulizungumze”
Tukaagana na Manka kisha mimi nikaondoka na kumuacha akazungumza na ndugu zake kisha,Nikakodi boda boda ya pikipiki hadi nyumbani nikamuacha jamaa getini nikingia chumbani kwangu kumchukulia pesa ambayo ilipungua kwenye malipo yake kisha nikarudi ndani na kumkuta mama sebuleni akionekana akinisubiri.Nikaanza kupandisha ngazi za kwenda ndani kwangu.
“Wewe Eddy”
“Naam”
“Hebu shuka hapa”
Nikashuka na kukaa kwenye moja ya sofa kisha na yeye akakaa kwenye sofa jengine.
“Hebu wewe mtoto niambie ni nani aliye kupiga risasi?’
“Mama kile nilicho kizungumza mahakamani ndio hicho hicho”
“Ila Eddy manangu kwanini siku ya kwanza nilivyo kuuliza ukasema Manka ndio muhusika?”
“Hapana labda nilikosea”
“Kukosea tena mwanangu…..Ila na kwanini ulisema umetembea na Manka?”
“Ahaaa mama ulinisikia vibaya”
“Eddy Eddy mwanangu jua kuwa mimi ni mtu mzima na kila unachopitia,mimi pia nilishapitia kipindi ninakua sasa usitake kunidanganya hebu niambie ukweli mwanangu ni kweli Manka ulitembea naye?”
“Sijatembea naye wewe si umesema ni dada yangu?”
“Ndio ni ndugu yako……Kachukue begi lako la nguo dereva akupeleke shule”
Mama jioni yote hii dereva anipeleke shule?”
“Maamuzi ndio hayo kavae nguo zako za shule dereva akupeleke Arusha”
“Lakini mama sijapona vizuri”
“Hujapona vizuri au unataka kujidekeza dekaza kumbuka kuwa wewe ni A level tena mwenyewe unajiita PCB sasa sijui huko shule kama unasoma au ndio kurukaruka vaa upelekwe shule”.
Kitendo cha mama kuniambia nijiandae nirudi shule kikanikosesha amani katika moyo wangu na sikuwa na jinsi zaidi ya kujiandaa na taratibu ili dereva anirudishe.Hadi namaliza kujiandaa ikawa imeshatimu saa kumi na moja jioni.Nikabeba begi langu la nguo na kulipakiza ndani ya gari.
“Eddy nataka huko shule ukasome sihitaji michezo ya kijinga jinga tambua kuwa wewe umesha kuwa mtu mzima unapaswa kuaanza kufikiria maisha yako na ya wanao ila sio kufanya ujinga kama ulio ufanya”
“Sawa mama”
“Kama mutakuwa munachelewa mutalala kwenye Hotel yoyote njiani”
“Sawa”.
Mama akanipa kiasi cha kutosha cha matumizi ya pesa ya kutumia shukeni pamoja na pesa ya matumizi njiani na safari ikaanza,kutokana na foleni iliyopo jijini Dar es salaam ikatifanya tusimame simame san njiani
“Kaka naomba niendeshe niendeshe gari”
“Ningekupa mdogo wangu ila huna leseni”
“Kwani usiku huu ni trafki gani atakaye tusimamisha njiani?”
“Mbona wapo wengi hii ni barabara ya mkoani ni lazima tutawakuta wengi”
“Sawa”
Safari ikaendelea huku nikiwa nimelala kwenye siti ya gari na kumuacha dereva kufanya kazi yake.Dereva akaniamsha na nikakuta tumesha fika katika sehemu moja inaitwa Mombo kwenye hoteli moja inaitwa Liverpool,tukaingia na kuapata chakula cha usiku na tukarudi dani ya gari na safari ikaanza.Kutokana sikuwa na mazoea na huyu dereva mpya wa mama nikaona ni bora kulala kwani sikuwa na chakuzungunza naye.
Nikastushwa na breki kali za gari letu na kunifanya nishtuke na nikamkuta dereva akijitahidi kuikwepa gari ndogo aina ya PREMORE inayopinduka pinduka katikati ya barabara.Gari ikatulia na kuingia ndani ya mtaro ikamlazimu dereva kulisimamisha gari letu mbele kidogo kutoka sehemu gari ndogo ilipo angukia.Mimi na dereva tukajikuta tumetulia kama kwa dakika tano huku kwa upande wangu mapigo ya moyo yakinienda mbio kiasi kwamba nikashindwa nifanyaje.
“Kaka imekuwaje?”
“Mmmmmm?”
“Imekuwaje?”
“Nilikuwa ninamuomba dereva wa lile gari anipishe njiani ila akawa anashindana na mimi katika akukimbiza gari…..ila kutokana na taa za gari zangu kuwa uwezo mkubwa basi nikajikuta ninamuwashia zote ndio jamaa akaanza kijichanganya changanya hadi akadondoka”.
“Mmmmm huu msala tusepe zetu basi”
“Mmmm siwezi hata kuendesha gari”
“Ngoja mimi nije kuendesha”.
Nikashuka ndani ya gari nikiwa ninazunguka nyuma kwenye gari ili niiingie kwenye siti ya dereva nikapata mshtuko baada ya kumuona msichana akianza kujivuta taratibu kutoka ndani ya gari huku akilia kwa maumivu makali ikanibidi nianze kupiga hatua za kwenda kumsaidia ila kadri jinsi nilivyozidi kwenda moyo ukazidi kunipasuka kwani mtu anaye jitahidi kujitoa ndani ya gari ni Manka....
ITAENDELEA......
RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 14
4/
5
Oleh
Unknown